Kufanya Ukaguzi wa mara kwa mara wa Skuli na mwalimu mmoja mmoja kama ilivyofafanuliwa katika Mfumo wa Ukaguzi uliowekwa na Ofisi.
Kuhakikisha kuwa mtaala uliokubalika ndio unaotumika kwa ajili ya kuleta ufanisi wa utoaji wa elimu katika skuli.
Kuweka Viwango vya Ukaguzi na viashiria vya utekelezaji ili kudumisha ubora wa Skuli katika masuala ya uongozi na uendeshaji, ufundishaji na ujifunzaji, msaada kwa wanafunzi na matokeo ya kujifunza.
Kushajihisha matumizi ya teknolojia ya habari na mawasilino kwa lengo la kuongeza ufanisi katika ukaguzi wa elimu.
Kuzielekeza skuli zilizokaguliwa juu ya mambo yanayohusu uimarishaji wa elimu bora kwa kuzingatia taarifa za utendaji wa skuli na ripoti za ukaguzi.
Kutoa Ripoti ya kila mwaka ya ukaguzi wa elimu na kutoa mrejesho wa uthibiti ubora kwa wadau wa elimu.
Majukumu ya Kitengo Uhasibu
Kuandaa na kufanya malipo mbalimbali ya Ofisi
Kuandaa taarifa za mapato na matumizi kwa kila mwezi, robo mwaka, nusu na mwaka kwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Fedha.
Kutayarisha hati za malipo kwa watumiaji kwa mujibu wa kasma za mgao wa Ofisi.
Kuandaa malipo na kuyawasilisha katika mifuko na makato maalum ya watumishi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu zinazohusika.
Kufuatilia upatikanaji wa fedha zilizotengwa.
Kufanya usuluhisho wa hesabu za Ofisi (Bank Reconciliation).
Majukumu ya Kitengo Cha Manunuzi
Kuandaa na kutekeleza mpango wa ununuzi wa mwaka wa Ofisi na kuandaa taarifa ya utekelezaji wake.
Kufanya tathmini ya uchakavu wa vifaa na samani za Ofisi, kuamua mwisho wa matumizi yake na kuvifuta kwenye daftari la mali za Ofisi.
Kuandaa daftari la mali za Ofisi.
Kuandaa mapendekezo ya bajeti ya kitengo ya kila mwaka
Kuandaa zabuni na kuratibu usimamizi wa utekelezaji wake.
Kununua, kutunza na kusimamia usambazaji wa vifaa na huduma mbalimbali za Ofisi kwa mujibu wa Sheria na Miongozo ya Ununuzi.
Majukumu ya Kitengo cha Sheria
Kutoa ushauri juu ya masuala yote ya kisheria na kusaidia katika kutoa tafsiri juu ya sheria na mikataba mbalimbali kwa Ofisi ili kuliwezesha kutekeleza majukumu yake.
Kushiriki na kutoa ushauri wa kisheria wakati wa majadiliano mbalimbali yanayohusu Mamlaka juu ya makubaliano au mikataba maalumu.
Kuandaa mapendekezo ya bajeti ya kitengo ya kila mwaka.
Kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa Sheria na taratibu mbalimbali katika Ofisi na kutoa ushauri ili kuziboresha zaidi
Kushirikiana na Mwanasheria Mkuu katika kushtaki na kuendesha kesi za madai.
Kuandaa nyaraka mbali mbali za kisheria
Majukumu ya Kitengo cha TEHAMA
Kushauri juu ya mambo yanayohusiana na teknolojia ya habari na mawasiliano.
Kutayarisha na kusimamia tovuti ya Ofisi.
Kuhifadhi na kusimamia kumbukumbu, taarifa na nyaraka zote zilizomo katika hati laini (soft copies)..
Kuandaa na kusimamia data base ya Ofisi
Kuandaa na kutekeleza mkakati wa mawasiliano wa Ofisi.
Kuratibu uandaaji wa taarifa na nyaraka mbalimbali za Ofisi kusambaza nyaraka, vipeperushi, vitabu na taarifa za kielektroniki