Dhamira Yetu
Kufanya ukaguzi wenye Ubora wa juu, unaozingatia Sera, Sheria, Mitaala na viwango vya elimu ili Kuthibiti Ubora na kunyanyuwa kiwango cha Elimu inayotolewa katika Skuli zote za Zanzibar.
Lengo
Kuisaidia Serikali na Sekta binafsi katika kuimarisha utendaji wa watumishi wake katika utoaji wa elimu bora kwa umma ili kusaidia mageuzi yanayoendelea katika sekta ya elimu
Maadili Yetu
Uaminifu na Uadilifu, Usiri katika kazi, Nidhamu, Uwajibikaji, kufanya maamuzi yanayotegemea ushahidi na kutoa huduma kwa maslahi ya Taifa
Ndg: Maimuna Fadhil Abass
Nina furaha kubwa na shukrani
kuwakaribisha kwenye tovuti yetu.
Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu Zanzibar
(OCIE)
Kuhusu Taasisi
Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu Zanzibar ni Taasisi ya Serikali chini ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar iliyoundwa kwa mujibu wa Sheria ya Kuanzisha Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu Namb. 10 ya mwaka 2018. Ofisi hii hutumia ufupisho wa Kiengereza OCIE (The Office of Chief Inspector of Education).
Awali ilikuwa Idara ya Ukaguzi wa Elimu Zanzibar. Ili kukidhi vyema dhima ya Ofisi hii, ilibadilishwa kutoka Idara ya Ukaguzi na kuwa Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu Zanzibar mwaka 2011.
Ofisi hii imeanzishwa kwa malengo ya kuhakikisha kuwa elimu inatolewa kwa mujibu wa sera, sheria na miongozo ya Serikali na taasisi zinafundisha kwa mujibu wa mitaala iliyoidhinishwa kwa ngazi husika. Vile vile kuhakikisha kuwa miiko na maadili ya kazi ya Ualimu inafuatwa, kushauri juu ya viwango bora vya uendeshaji wa skuli, ufundishaji na ujifunzaji, kuwasaidia wanafunzi pamoja na kutumia zana sahihi za upimaji.
Matangazo
Mafunzo ya Muongozo wa Ukaguzi wa Vyuo vya Ualimu kwa Wakaguzi wa Elimu wa Mikoa ya Unguja
Kiembe Samaki TCMafunzo ya Muongozo wa Ukaguzi wa Vyuo vya Ualimu kwa Wakaguzi wa Elimu wa Mikoa ya Pemba
Michakaeni TCUwasilishwaji wa Ripoti ya Tathmini ya Ukaguzi ya Mwaka 2024/2025 Mkoa Kaskazini Unguja
Afisi ya Elimu Wilaya Kaskazini "B" , Mkwajuni Tazama Uwasilishaji wa RipotiUkaguzi wa Skuli
kuangalia mazingira salama, mtaala unaofaa kwa watoto wadogo, na mbinu shirikishi za ufundishaji.ili kuhakikisha msingi mzuri wa kusoma, kuandika, na kuhesabu
Utekelezaji wa mtaala, ushiriki wa wanafunzi, uwiano wa walimu kwa wanafunzi, na upatikanaji wa vifaa vya kujifunzia ili kuhakikisha watoto wanapata maarifa yatakayowasaidia.
Ubora wa ufundishaji, ufanisi wa walimu, matumizi ya teknolojia, na usimamizi wa nidhamu kwa maandalizi ya elimu ya juu pamoja na soko la ajira
Habari na Matukio
13 June 2026
Dkt.Mpango Primary School, PembaWakaguzi wa Elimu na Washirika wa Vyuo vya Ualimu Pemba Wanolewa Juu ya Mwongozo Mpya wa Ukaguzi . ...
Soma zaidi
15 May 2026
Baraza la Wawakilishi, ZanzibarWaziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Lela Muhamed Mussa akiwasilisha Bajeti ya Wizaya ya Elimu ...
Soma zaidi
13 May 2026
Afisi ya Elimu Wilaya Kaskazini B, UngujaUwasilishwaji wa Ripoti ya tathmini ya Ukaguzi ya Mwaka 2024/2025 Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Soma zaidi